Wednesday, December 23, 2015

Serikali yawajengea uwezo walimu wa sekondari Lindi na Mtwara.

Walimu kutoka katika shule mbalimbali za sekondari za mikoa ya Lindi na Mtwara wakiwa katika mafunzo ya kuwajengea uwezo kwa ajili ya kuinua kiwango cha ufaulu kwa masomo manne ya Hisabati, Kiswahili, Baiolojia na Kiingereza, yalioandaliwa na Ofisi ya Rais (TAMISEMI) kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, na kufanyika katika ukumbi wa shule ya sekondari ya wasichana Masasi


Na Juma Mohamed.

KATIKA kuendeleza utekelezaji wa mpango wa Matokeo Makubwa Sasa, serikali kupitia Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), inaendesha mafunzo kwa walimu wa shule za sekondari katika mikoa ya Lindi na Mtwara kwa ajili ya kuwajengea uwezo katika masomo ya Hisabati, Baiolojia, Kiswahili na Kiingereza.
Akizungumza juzi na waandishi wa habari, afisa elimu kutoka idara ya usimamizi wa elimu ofisi ya Rais TAMISEMI Dodoma, Hellen Msellem, ambaye pia ni mratibu wa mafunzo hayo, alisema mafunzo hayo yamewekwa mahususi kwa ajili ya kuinua kiwango cha ufaulu katika masomo hayo ambayo katika miaka mitatu iliyopita wanafunzi walionekana kuto fanya vizuri.
Alisema, kutokana na mwaka huu kiwango cha ufaulu kuwa ni asilimia 80, imewekwa mikakati itakayowawezesha walimu na wanafunzi kufikia malengo, ambapo miongoni mwake ni pamoja na huo wa kutoa mafunzo kwa baadhi ya walimu ili na wao waende kuwafundisha walimu wengine.
“Na kwa mwaka huu kama sijakosea kiwango cha ufaulu kilichowekwa ni asilimia 80, sasa ili kuweza kuifikia hiyo kuna malengo ambayo yamewekwa, moja wapo ni hili la kuwawezesha walimu ili waweze kuangalia yale masomo ambayo watoto wanaonekana wako chini katika ufaulu yaweze kuboreshwa katika ufundishwaji na hatimae kuna wale wanafunzi ambao wana uwezo mdogo kwenye hayo masomo waweze kupewa masomo yaziada..” alisema.
Kwa upande wao, baadhi ya walimu wanaoshiriki mafunzo hayo, waliiomba serikali kuto ishia katika masomo hayo manne pekee, isipokuwa mpango huo uendelee katika masomo mengine kwani kwa kufanya ivyo itasaidia kwa kiasi kukubwa kuondoa tatizo la kufeli kwa wanafunzi wengi hapa nchini.
“Jambo hili ni zuri sana na naiomba serikali tusiishie tu katika masomo haya manne ya Baioliji, Mathematics (Hisabati), Kiswahili na Kiingereza..watakapopata fursa kama hii na wakawezeshwa kama tunavyowawezesha ambapo sasa tunauwezo wa kuwapambanua au kuwatambua wale wazito kwa hizi hatua tulizofundishwa na hawa wawezeshaji, kwahiyo itatuwezesha kubaini mapungufu ya motto, namna ya kumsaidia na mwisho wa yote tutafuta ufaulu wa daraja sifuri muda mfupi ujao..” alisema mwalimu Khalidi, kutoka shule ya sekondari ya Michiga, wilayani Nanyumbu.



No comments: